Zoezi la Uandikishaji na Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, Jimbo la Arumeru Magharibi linaendelea vema kwenye vituo vyote 238 vilivyopangwa huku vijana wakijitokeza zaidi.
Katika vituo vilivyotembelewa na mwandishi wetu, vijana wengi walikuwa kwenye vituo vya kujiandikishia daftari la kudumu la wapiga Kura, jambo linalothibitisha, mwitikio chanya kwa vijana, hasa kwa kuzingatia kundi hilo liliachwa mwaka 2015 kutokana na kigezo cha umri, wakati vijana hao sasa wamepata sifa, ambapo wapo wanaofikisha miaka 18 sasa na wapo wanaotarajia kufikisha miaka 18 ifikapo tarehe 28.10.2020.
Baadhi ya vijana wamesema kuwa wakati wa uandikisha wa Daftari la kudumu la wapiga kura, uliofanyika mwaka 2014, walikuwa hawajatimiza umri wa miaka 18, lakini sasa umri unawaruhusu kuwa wapiga kura halali.
Julias Laiza, mwenye miaka 20 amesema kuwa wakati wa uandikisha mwaka 2015, alikua na umri wa miaka 16 hivyo hakuwa na sifa za kujiandikisha, lakini sasa umri umefika na kupata sifa za kujiandikisha.
Aidha tuwatake wananchi wote wenye sifa, kujitokeza kujiandikisha kwenye Daftari la kudumu la wapiga kura ili upate Kadi, itakayokuwezesha kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu ujao, unaotarajiwa kufanyika mapema mwezi Oktoba 2020.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.