Na. Elinipa Lupembe.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt.John Pombe Magufuli, amewashukuru watanzania wote kwa kukubali wito wa kuacha kutumia mifuko ya plastiki na kuanza kutumia mifuko mbadala iliyoelekezwa na Serikali.
Rais Magufuli ametoa shukurani hizo, wakati akiwa kwenye matembezi yake ya jioni katika Soko la Samaki Ferry jijini Dar es salaam na kuzungumza na wafanyabiashara wa Samaki katika Soko hilo, kuhusu umuhimu wa kutumia mifuko mbadala na kuachana na kutumia mifuko ya plastiki.
Rais pia, amepata fursa ya kuelezea madhara makubwa yanayotokana na matumizi ya mifuko ya plastiki kwa binadamu na kwenye mazingira ya nchi yetu, ikiwemo mazingira ya baharini na viumbe vyake, madhara kwa mifugo na wanyamapori pamoja na ardhi kupoteza uhalisia wake unaotokana na mifuko hiyo kutokuoza mara baada ya kutupwa.
Aidha Rais Dkt. Magufuli mara baada ya kuzungunza na wafanyabiashara hao, alinunua samaki katika soko hilo na kuwahifadhi katika kikapu chake cha kiasili, kitendo ambacho kimethibitisha kuwa, Tanzania bila mifuko ya plastiki inawezekana.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akinunua samaki kwa mmoja wa wafanya biashara wa samaki, kwenye soko la Ferry Jijini Dar es Salaam alipotembelea sokoni hapo.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.