Mkuu wa mkoa wa Arusha, mheshimiwa Mrisho Gambo anapenda kuwajulisha wananchi wa wilaya ya Arumeru kuwa, kutakua na ugeni wa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli katika Halmashauri ya Arusha, wilayani Arumeru, kesho Jumapili tarehe 02.12 2018 kwenye kata ya Kimnyaki.
Akiwa katika kata ya Kimnyaki, Mheshimiwa Rais, ataweka Jiwe la Msingi kwenye ujenzi wa Visima vya Maji, Visima ambavyo ni vyanzo vya mradi mkubwa wa maji unaotekelezwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jiji la Arusha (AUWSA) wenye thamani ya shilingi bilioni 520, mradi unaotarajiwa kupunguza tatizo la maji katika Jiji la Arusha pamoja na maeneo ya jirani ya wilaya ya Arumeru ambako ndiko kwenye chanzo kikuu cha maji.
Mara baada ya kuweka Jiwe la Msingi la ujenzi huo wa Visima vya Maji, Mheshimiwa Rais, atazungumza na wananchi wilaya ya Arumeru kwenye mkutano wa hadhara, utakaofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Olimringaringa.
Katika ziara hiyo Mheshimiwa Rais ataambatana na viongozi mbalimbali wa Serikali.
Wananchi wote mnaombwa kuhudhuria, kwenye Mkutano huo wa hadhara na kumsikiliza Rais wenu wa Serikali ya awamu ya tano, Serikali inayowajali wananchi.
MUDA: KUANZIA SAA MBILI KAMILI ASUBUHI
'HAPA KAZI TUU - TUNATEKELEZA'
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.