Watalamu wakaguzi wa nyama halmashauri ya Arusha wamelazimika kuzuia ulaji wa nyama ya ng'ombe aliyechinjwa na kupimwa na kugundulika kuwa na dalili za ugonjwa uliosababisha ini kushindwa kufanya kazi.
Daktari wa Mifugo halmashauri ya Arusha Dkt, Linus amesema kuwa ng'ombe huyo alichinjwa katika machinjio ya Sanawari na baadaye kupimwa nyama yake na hatimaye kuzikwa mara baada ya madaktari hao wa mifugo kugundua nyama hiyo hafai kwa matumizi ya binadamu.
Dkt. Linus amesema kuwa wamelazimika kufukia nyama ya ng'ombe huyo baada ya kuthibitika kuwa na ugonjwa uliosababisa ini kushindwa kufanya kazi na amefafanua kwa lugha ya kitaalamu kuwa ni icterus, haemorrhage, multiple hepatic abscesses.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.