Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha Dk. Wilson Mahera ametumia muda wake kuwafundisha wanafunzi wa kidato cha II shule ya Sekondari Oldonyosambu somo la Kemia.
Dk. Mahera amefanya marudio kwenye mada ya 'Elements' baada ya kutembelea shuleni hapo kwa shughuli zake za kikazi na kuwakuta wanafunzi wakiwa kwenye maandalizi ya mtihani wa uzamilifu utakaoanza Jumatatu ijayo tarehe 21.08.2017.
Awali mkurugenzi huyo alianza kuwauliza maswali ya somo la Kemia baada ya wanafunzi kujibu maswali hayo kwa kusuasua alijikuta akianza kuwafundisha mada hiyo maarufu kama 'First 20 elements' ambayo ni mada ya msingi kwa wanafunzi wa kidato cha pili.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.