Watalamu wa halmashauri ya Arusha kwa kushirikiana na wataalamu Washauri wa Don Consult Ltd wamefanya Mkutano na viongozi wa serikali, wazee wa mila na koo, watu mashuhuri wa kitongoji cha Ngaramtoni kata ya Olmotony kwa ajili ya kuutambulisha mradi wa maji utakaotekelezwa na shirika lisilo la kiserikali la WaterAid mradi unaoanza Julai 2017 mpaka Mei 2018.
Wakati wa mkutano huo watalamu wamepata fursa ya kuutambulisha mradi huo wa maji pamoja na kuielezea jamii umuhimu wa maji katika jamii, utunzaji wa mazingira ya vyanzo vya maji, usafi wa mazingira na usafi wa maji.
Hata hivyo walipata fursa ya kuuelezea uchangiaji wa matumizi ya maji hayo kwa kutumia mfumo wa kielektroniki wa kulipia kabla ya kutumia 'eWater paid' ili wananchi wafahamu uchangiaji wa huduma hiyo.
Jamii inapaswa kutambua kuwa mradi huu wa maji utaenda sambamba na utunzaji wa mazingira na ujenzi wa vyoo vya mfano kwenye taasisi na maeneo ya huduma za jamii kadri itakavyopendekezwa.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.