Na. Elinipa Lupembe.
Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Saad Mtambule, amewataka watumshi, halmashauri ya Arusha, kuendelea kufanya kazi kwa bidii, na kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia kanuni na sheria na taratibu za kazi, licha ya changamoto zinazowakabili katika utumishi wao na katika maeneo yao ya kazi.
Mkurugenzi Mtambule ameyasema hayo, wakati akifungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi, halmashauri ya Arusha, wakati wa mkutano wa kupitia na kujadili rasimu ya bajeti ya mwaka ujao wa fedha 2021/2022, mkutano unaofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.
Imeelezwa kuwa serikali inaendelea kutatua changamoto za watumishi licha ya kwamba si rahisi kuzimaliza zote kwa wakati mmoja, na kuwataka watumishi hao, kuendelea kujituma katika kufanya kazi na kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia kanuni, sheria na taratibu za utumishi wa Umma.
"Watumishi wa umma bado wanachangamoto nyingi lakini serikali inaendelea kutatua changamoto hizo na kuzipunguza kwa kupunguza ukiritimba uliokuwa unakwamisha baadhi ya mambo, na hata hivyo itachukua muda mrefu kuzimaliza changamoto hizo" amesisitiza Mkurugenzi huyo.
Mkutano huo wa Baraza la Wafanyakazi, umefanyika kwa mujibu miongozo ya serikali za mitaa, kushiriki katika mchakato wa maandali ya bajeti ya halmashauri.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.