Bweni la wasichana shule ya sekondari Mwandeti limeungua moto na kusababisha uharibifu wa jengo hilo, pamoja na hasara ya vifaa na mbalimbali vya wanafaunzi wanaolala katika bweni hilo, ikiwemo vitanda na magodoro.
Mkuu wa shule ya sekondari Mwandeti, mwalimu John Masawe, amesema kuwa moto huo umesababisha taharuki kwa wanafunzi wa shule hiyo, na kusababisha hasara ya kuteketea kwa vitanda, magororo, vifaa binafsi vya wanafunzi pamoja na uharibifu wa jengo.
Hata hivyo, Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Selemani Msumi licha ya kusikitishwa na ajali hiyo ya moto ambayo imesababisha hasara na taharuki kwa wanafunzi, amewataka wanafunzi hao, kuwa watulivu wakati serikali ikiendelea na taratibu nyingine, ikiwemo kuchunguza chanzo cha ajali hiyo pamoja na kukarabati jengo hilo.
Aidha mkurugenzi Msumi, amethibitisha kuagiza timu ya watalamu waliofanya tathmini ya uharibu uliotokea, na tayari halmashauri imeshatoa kiasi cha shilingi milioni 5 kwa ajili ya kununulia baadhi ya vifaa, tayari kwa kuanza matengenezo ya awali.
"Kiasi hicho cha fedha kitatumika kununu baadhi ya vifaa vya kukarabari vitanda, kununua gipsam, na alminium, vifaa ambavyo vitasaidia katika hatua za awali za ukarabati wa bweni hilo" amefafanua Mkurugenzi Msumi.
Naye Afisa wa Polisi wa kikosi cha zima moto Jiji la Arusha Geradi Nonkwe amesema kuwa, kikosi hicho kinaendelea kuchunguza chanzo cha ajali hiyo, kwa kuwa bado hakijajulika na kuwataka, wananchi kuendela kuchukua tahadhari ya moto katika maeneo yao.
Mkurugenzi mtendaji halamshauri ya Arusha, anatoa pole kwa wanafunzi na jumuia ya nzima ya shule ya sekondari Mwandeti, na kuwataka wadau wa elimu kujitokeza kusaidia ukarabati wa bweni hilo la wasichana kwa ajili ya kuwezesha wanafunzi kuendelea masomo yao katika hali ya kawaida.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.