Katika kuendelea kubuni miradi ya kuingozea mapato na kuiwezesha halmashauri kuendesha shughuli zake bila mkwamo wa kipesa, hamalmashauri ya wilaya ya Arusha wilayani Arumeru, imekabidhiwa gari la kubebea mitambo na mizigo mizito, aina ya Foton Auman, gari lililonunuliwa na halmashauri hiyo kupitia kampuni ya uuzaji magari ya Simba Motors, katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Ofisi za makao maku ya halmashauri hiyo, eneo la Sekei.
Halmashauri hiyo imeendelea kupata neema ya magari kwa mwezi huu wa Novemba, 2018, ikiwa gari hilo ni la sita kupokelewa na Halmashauri hiyo, baada ya kupokea msaada mwingine wa magari matano, mapema wiki mbili zilizopita kutoka kwa kikundi cha Friend of German cha nchini Ujerumani, licha ya kuwa gari hilo limenunuliwa na halmashauri hiyo.
Akizumgumza wakati akikabidhi kadi na funguo za gari hilo kwa uongozi wa halmashauri ya Arusha, Mkurugenzi wa Kampuni ya Simba Motors, Brigedia Generali mstaafu, Maiko Luhongo amesema kuwa gari hilo ni jipya na limeagizwa kutoka kiwandani moja kwa moja na kuutaka uongozi wa halmashauri kulitunza gari hilo kwa kuajiri, dereva mwenye sifa nauzoefu wa kuendesha magari makubwa ,waminifu na mwenye nidhamu ya kazi.
Mwenyekiti wa halmashaui ya Arusha, mheshimiwa Noah Lembris, amewapongeza wataalamu wa halmashauri ya Arusha, waliowezesha kupatikana kwa gari hilo, wakiongozwa na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Dkt. Charles Mahera, kwa kuwa lengo la kununua gari ni pamoja na kuongeza wigo wa upatikanaji wa mapato ya halmashauri.
Mwenyekiti huyo, amewataka watumishi wote wa halmashauri, kushirikiana kwa pamoja kulitunza gari hilo ili liweze kufanyakazi kwa ufanisi na kuzalishak jambo ambalo ndilo lilikuwa kusudi kubwa la kumiliki gari hilo.
Naya Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Dkt. Wilson Mahera, amefafanua kuwa, gari hilo litakuwa likikodishwa pamoja na kufanya kazi ya kusafirisha mitambo ya halmashauri hiyo inayotumika kutengeneza barabara za ndani ya halmashauri ikiwa ni utekelezaji wa kazi za jamii.
Ameongeza kuwa, gari hilo litatumika kama chanzo cha mapato ya ndani ya halmashauri yao na kuthibitisha kuwa upatikanaji wa mapato hayo, utawezesha kutatua changamoto zinazowakabili wananchi katika sekta ya elimu, afya, maji pamoja na miundombinu ya barabara.
Hata hivyo Dkt. Mahera amewataka wananchi pamoja na wadau wa ndani na nje ya halmashauri hiyo, kujitokeza kwa wingi kwaajili ya kukodi gari hilo kwa kufanyia shughuli mbalimbali ili waweze kuimarisha mapato ya halmashauri yake.
“Niwaombe wananchi na wadau mbalimbali mjitokeze kwa wingi kukodi gari hili, kwaajili ya kuwasaidia kufanya shughuli zenu kwani mkifanya hivyo mtakuwa mmeisaidia halmashauri yetu, kuongeza mapato ambayo yatasaidia kutatua changamoto zinazowakabili wananchi wa hali ya chini” alisema Dkt.Mahera.
Mradi huo wa gari ni moja kati ya miradi inayotekelezwa na halmashauri ya Arusha yenye lengo la kuongeza pato la halmashauri na hatimaye mapato hayo kutumika kutatua changamoto zinazowakabili wananchi wa halmashauri hiyo pamoja na kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano za kutaka kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.
Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha mhe. Noah Lembris (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Dkt. Wilson Mahera, wakikata utepe ishara ya kuzindua gari na SM 12581 mara baada ya kukabidhiwa na Kampuni ya Simba Motors iliyopata zabuni ya kuwauzia gari hilo.
Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Dkt. Wilson Mahera, akionyesha kadi na funguza za gari namba SM 12581 mara baada ya kukabidhiwa na Kampuni ya Simba Motors iliyopata zabuni ya kuwauzia gari hilo.
Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha mhe. Noah Lembris, akiliwasha gari la halmashauri hiyo, mara baada ya kukabidhiwa na Kampuni ya Simba Motors iliyopata zabuni ya kuwauzia gari hilo.
Watumishi wa halmashauri ya Arusha, wakiwa kwenye hafla ya kupokea gari la halmashauri ya Arusha.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.