TANGAZO LA URASIMISHAJI ARDHI /MAKAZI ENEO LA KISERIANI
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha, anawakumbusha wananchi wote wenye ardhi katika eneo la Kiseriani kata ya Mlangarini, kuwa zoezi la URASIMISHAJI ARDHI/MAKAZI linaendelea katika maeneo hayo, hivyo wananchi hao wanatakiwa kujitokeza kwenye OFISI YA KIJIJI CHA KISERIANI AU OFISI YA ARDHI HALMASHAURI YA ARUSHA ENEO LA SEKEI ili kutoa taarifa zao.
Aidha anawataka wale wote ambao maeneo yao tayari yametambuliwa kulipia gharama za URASIMISHAJI kiasi cha Tsh. 150,000/- ndani ya miezi miwili kuanzia tarehe 01, Januari mpaka 28, Machi 2021 ili taratibu za upatikanaji wa HATI MILIKI zianze na zikamilike kwa muda uliopangwa.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.